Kapinga: Maeneo ya kijamii yamepewa kipaumbele kufikiwa na umeme

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri Nishati, Judith Kapinga amesema utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini umetoa kipaumbele kwenye maeneo yanayotoa huduma za kijamii ikiwemo Shule, Taasisi, vituo vya afya, zahanati na maeneo ya visima vya maji kwa sababu ni maeneo yanayotoa huduma kwa jamii.

Kapinga ameyasema hayo leo Machi 18, 2025 katika Vijiji vya Lwangu na Welela vilivyopo katika Halmashauri ya Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kukagua miradi ya umeme vijijini pamoja na kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kipaumbele ni Taasisi kwa sababu zinatoa huduma zinazotunufaisha sisi wote, tunataka umeme ukatumike kwenye vituo vya afya, zahanati, kwenye visima vya maji lakini pia kwenye shule,” amesema.

Ameongeza kuwa, kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini hufanyika tathmini ili kuyabaini maeneo yanayotoa huduma za kijamii huku akibainisha hakuna maeneo yanayo rukwa.

spot_img

Latest articles

DIB yawahakikishia wananchi usalama wa amana zao

Na Mwandishi Wetu BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewahakikishia wananchi kuwa fedha wanazoweka...

DAWASA MTAA KWA MTAA KUTATUA CHANGAMOTO ZA HUDUMA

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

UKAGUZI WA MIGODI WAIMARISHA USALAMA, UHIFADHI WA MAZINGIRA

Tume ya Madini yasisitiza uchimbaji unaozingatia sheria, afya na maendeleo endelevu Na Mwandishi Wetu...

Mhitimu wa VETA abuni mashine ya kupunguza gharama za ufugaji na kuongeza thamani ya mazao

Na Mwandishi Wetu MHITIMU wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia VETA, Ernest Maranya, amebuni mashine...

More like this

DIB yawahakikishia wananchi usalama wa amana zao

Na Mwandishi Wetu BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewahakikishia wananchi kuwa fedha wanazoweka...

DAWASA MTAA KWA MTAA KUTATUA CHANGAMOTO ZA HUDUMA

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

UKAGUZI WA MIGODI WAIMARISHA USALAMA, UHIFADHI WA MAZINGIRA

Tume ya Madini yasisitiza uchimbaji unaozingatia sheria, afya na maendeleo endelevu Na Mwandishi Wetu...