BEKI WA YANGA APANDISHWA CHEO AWA SAJENTI

Na Mwandishi Wetu

Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM), kimempandisha cheo mchezaji wetu Ibrahim Hamad “Ibra Bacca” kutoka Koplo na kuwa Sajenti kutokana na kuonesha kiwango bora Uwanjani.

Akizungumza baada ya kupandishwa cheo hicho, amesema anakishukuru kikosi chake kutokana na sapoti wanayoitoa kwake kila sehemu anayopita na kuahidi kuendelea kuitumikia nchi yake.

“Sina budi kushukuru kikosi changu kwa kuweza kunisapoti kwa kila hatua. Nitaendelea kuipambania nchi yangu,” amesema Sajenti Ibrahim Bacca ambaye wazazi wake pia ni askari.

Beki huyo alisajiliwa na Yanga  msimu wa  2022/2023 kutoka KMKM  ambacho ni  kikosi cha ulinzi cha Zanzibar ambacho kina jukumu la kulinda mipaka ya bahari dhidi ya magendo, uvuvi haramu, na vitendo vingine vya kihalifu. Pia, KMKM husaidia katika operesheni za uokoaji baharini na usalama wa majini.

spot_img

Latest articles

Waogeleaji wa Lake Victoria Sports Club waahidi kuing’arisha Tanzania Kimataifa

Na Mwandishi Wetu Jumla ya waogeleaji sita  chipukizi wa Lake Victoria Sports Club  ya jijini...

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...

Kafulila: Hatuwezi kujenga uchumi wa nchi bila kushirikisha sekta binafsi

Na Tatu Mohamed, Mwanza MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma...

More like this

Waogeleaji wa Lake Victoria Sports Club waahidi kuing’arisha Tanzania Kimataifa

Na Mwandishi Wetu Jumla ya waogeleaji sita  chipukizi wa Lake Victoria Sports Club  ya jijini...

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...