Benki ya Stanbic kuendelea kuzisaidia Kampuni ndogo za uchimbaji wa mafuta na gesi

Na Mwandishi Wetu

BENKI ya Stanbic imesema kuwa itaendelea kushirikiana na makampuni madogo ya Kitanzania yanayojishughulisha na uchimbaji wa mafuta na gesi katika kuwapa uzoefu katika miradi mikubwa ijayo.

Hayo yameelezwa leo Machi 06, 2025 na Makamu wa Rais wa Miundombinu ya Nishati, Joe Mwakenjuki katika Kongamano na maonesho ya Petroli ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25) amesema wameona makampuni ya watanzania yakijitokeza katika kuangalia fursa mbalimbali katika miradi ya mafuta na gesi.

Amesema Benki ya Stanbic imeweza kusaidia makampuni hayo madogo ya kizalendo katika mnyororo wa thamani kwenye shughuli zao za mafuta na gesi.

“Benki yetu imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia Kampuni ndogo za kitanzania katika kuwapa uzoefu katika miradi yao ya sasa wanayofanya ambayo ni midogo. Ni vema wenyewe kujipa uzoefu katika miradi ya sasa na sio kusubiri miradi mikubwa ya mafuta na gesi kufanya hata hii midogo wanaweza kufanya,” amesema Mwakenjuki.

Amefafanua kuwa Watanzania wanaendelea kujitokeza kwa wingi katika kuchangamkia fursa za miradi ya mafuta na gesi na kujiandaa na miradi mikubwa zaidi kuliko wanayotekelezwa kwa sasa.”Wanaweza kuja katika mabenki na kuweza kuwasaidia kupata uzoefu ili miradi mikubwa inapokuja tutaweza kuwasaidia zaidi kwani mahitaji ya kifedha,” amesema.

Amefafanua kuwa Stanbic Bank inashiriki kikamilifu katika kufadhili sekta ya mafuta na gesi barani Afrika kwa kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa njia endelevu na inatoa huduma za kifedha kama mikopo, biashara ya kifedha, na ushauri kwa kampuni zinazojihusisha na mafuta na gesi.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...