Rais Samia: Ujenzi Kituo cha kupoza umeme Handeni kuimarisha upatikanaji umeme

📌 Kituo kugharimu shilingi bilioni 50

📌 Zaidi ya Shillingi billioni 98 kutekeleza mradi wa gridi imara Kilindi

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema utekelezaji wa ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Handeni mkoani Tanga utakapokamilika utaboresha upatikanaji wa umeme katika Wilaya za Handeni na Kilindi pamoja na maeneo jirani.

Rais Samia ameyasema hayo leo Februari 25, 2025 katika ziara yake mkoani Tanga wakati akizungumza na wananchi wa Handeni mara baada ya kuzindua Shule ya Wasichana ya Kilindi na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

“Tatizo la umeme hapa Handeni Serikali inalifahamu, imeanza kuchukua hatua kwa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme kitakachogharimu takribani shilingi bilioni 50 za kitanzania ambacho kitaboresha upatikanaji wa umeme,” amesema Rais Samia.

Ameeleza kuwa, upatikanaji wa umeme wa uhakika Handeni utasaidia ukuaji wa uchumi pamoja na kuyainua madini ya kinywe ambayo yanapatikana Wilaya ya Kilindi na yanahitaji umeme wa kutosha.

Awali, Mbunge wa Kilindi, Omari Kigua aliishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 98 kwa ajili ya kutekeleza mradi ya gridi imara utakao husisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Mkata kupitia Handeni hadi Kilindi.

Kigua ameeleza kuwa Wilaya ya Kilindi ina Vijiji 102 ambavyo vyote vimefikiwa na umeme na sasa kazi inayoendelea ni ya kufikisha umeme kwenye Vitongoji.

spot_img

Latest articles

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

Tukatae kuingizwa kwenye ubwege wa kijamii

KATIKA siku za hivi karibuni nimemkumbuka sana Profesa Seithy Chachage (08.01.1955 – 09.07.2006). Huyu...

Tanesco yazindua rasmi zoezi la ulipwaji fidia kwa wananchi Lindi na Mtwara

📌 Lengo ni kupisha Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme 220kV Masasi,...

More like this

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

Tukatae kuingizwa kwenye ubwege wa kijamii

KATIKA siku za hivi karibuni nimemkumbuka sana Profesa Seithy Chachage (08.01.1955 – 09.07.2006). Huyu...