RAIS SAMIA: NAMRUDISHA MWANANGU JANUARI KWA MAMA, NILIMPIGA KOFI

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan amesema  anamrudisha Januari Makamba kwa mama kwani alimpiga kofi na kumfichia chakula  kama ilivyo desturi ya kina mama pindi mtoto anapomkera.

Rais Samia amezungumza hayo  leo Februari 24,2025 wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Lushoto mkoani, Tanga.

“Nataka nimuite mwanangu Januari hapa aje huku,arudi kwa mama, Sisi wamama mnatujua, ukimkera mama anakupiga kikofi, anakufichia chakula. Sasa mwanangu nilimpiga kikofi  na kumfichia chakula, lakini leo namrudisha kwa mama. Haya mwanangu njoo,” amesema Rais Samia huku akimkumbatia Makamba.

Katika hatua nyingine Rais Samia amezindua jengo la Halmashauri ya Bumbuli, wilayani humo na kusema kuwa madhumuni ya jengo hilo ni kusogeza huduma karibu ambapo na wananchi ambapo huduma zote zitakuwa zinapatikana humo.

spot_img

Latest articles

Humphrey Polepole ajiuzulu

Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubalozi na...

Nandy ahamasika kutangaza Nembo ya Made in Tanzania Kimataifa

Na Tatu Mohamed MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga (Nandy), amesema elimu aliyoipata...

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

More like this

Humphrey Polepole ajiuzulu

Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubalozi na...

Nandy ahamasika kutangaza Nembo ya Made in Tanzania Kimataifa

Na Tatu Mohamed MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga (Nandy), amesema elimu aliyoipata...

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...