FCS, Vodacom Foundation wasaini makubaliano kuelekea Wiki ya AZAKI

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Shirika la The Foundation for Civil Society (FCS), na  Vodacom Tanzania Foundatio wamesaini makubaliano ya mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya Shilingi milioni 150 ikiwa ni  udhamini  wa Wiki ya AZAKI 2024, itakayofanyika Jijini Arusha kuanzia Septemba 9 hadi 13, mwaka huu.

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini makubaliano hayo, iliyofanyika leo Mei 21,2024, Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Justice Rutenge, amesema kiasi hicho cha fedha kimeongeza chachu ya ushiriano wa pamoja wa kukuza maendeleo ya jamii kupitia Wiki ya AZAKi.

Aidha, katika kufanikisha Wiki ya AZAKi, FCS wamechangia shilingi milioni 250, ambapo michango mingine inatoka kwa wadau wa maendeleo zikiwemo asasi za kiraia.

Rutenge amesema kuwa ili kuweza kusonga mbele sauti mbalimbali za wadau na wabia zinahitaji katika kuchochea mchakato wa maendeleo.

“Ili tuweze kusonga mbele na kuiona Tanzania tunayoitaka, sauti za wadau na wabia mbalimbali zinahitajika kusikika na ziwe sehemu ya kutoa mchango katika mchakato mzima wa maendeleo ambayo yatasaidia kujenga maono ya kulipeleka Taifa letu mbele” amesema Rutenge.

Ameeleza kuwa Sekta Binafsi ni wabia na wadau wakubwa wa maendeleo, nakwamba ushirikiano huo ni muhimu katika kubadilishana uzoefu huku akibainisha kuwa FCS wamekuwa wabobezi na wenye uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Ushirikiano huu utasaidia kubadilishana uzoefu, Vodacom Foundation watanufaika na uzoefu tulionao katika kusimamia miradi ya maendeleo, kuchochea usawa wa makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo wanawake, vijana, watoto na watu wenye ulemavu. FCS nao watanufaika katika kuunganisha watu kwa kutumia teknolojia kwa kuzingatia nchi ipo kwenye mapunduzi ya teknolojia,” ameeleza Rutenge. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Foundation Tanzania, Zuweina Farah, amesema ili kufanikisha Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, ushirikiano wa pamoja unahitajika kati ya AZAKi, Sekta Binafsi na Serikali.

Pia ameongeza kuwa, lengo la Vodacom Foundation Tanzania ni kukuza ushirikiano katika kuleta maendeleo ya jamii, kuimarisha utawala bora na kuboresha mazingira ya Biashara nchini.

Wiki ya AZAKi mwaka huu imebebwa na kauli mbiu ya isemaho ‘Sauti, maono na thamani’ ambayo inaambatana na lengo Kuu la FCS la kuwezesha maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...