RAIS SAMIA AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUJIANDAA NA UDHIBITI WA ATHARI ZA ELNINO

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Taasisi mbalimbali za serikali kujiandaa mapema kukabiliana na mvua kubwa zinazotabiriwa nchini, ili kuepusha maafa na madhara kwa wananchi.

Rais Samia amesema taarifa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) zinaeleza uwezekano wa kuwepo kwa mvua kubwa zinazohusishwa na hali ya El Niño, hivyo viongozi wanapaswa kuchukua hatua za tahadhari mapema.

“Niwaombe nendeni mkajitayarishe, mkaweke mazingira sawa ili mvua hizo zitakapoanza zisilete maafa makubwa kwa wananchi wetu,” amesema.

Amesema tahadhari ambazo TMA imeanza kutoa zinapaswa kuchukuliwa kwa uzito na viongozi kuhakikisha mazingira yanaandaliwa ili kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua hizo.

“Kwa hiyo niwaombe sana, tahadhari zimeanza kutolewa, hatua zichukuliwe ili mvua hizi zisilete madhara kwa wananchi wetu,” amesema Rais Samia.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumamosi, Agosti 22, 2026, wakati akizungumza na wananchi Mkoani Pwani mara baada ya kuzindua Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Megawati 2,115 wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere.

spot_img

Latest articles

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

JNHPP kuongeza Umeme wa Gridi ya Taifa kwa asilimia 45

Na Tatu Mohamed BWAWA la Julius Nyerere (JNHPP) linatarajiwa kuongeza kwa kiasi kikubwa uwezo...

Tanzania kuandika historia leo, Rais Samia kuzindua Bwawa la Julius Nyerere

Na Tatu Mohamed TANZANIA inaandika ukurasa mpya katika historia ya sekta ya nishati leo...

RC Chalamila tafuta dozi ya Tume Keenja

KATIKA juhudi za kurejesha utawala wa sheria (orderly administration) katika jiji la Dar es...

More like this

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

JNHPP kuongeza Umeme wa Gridi ya Taifa kwa asilimia 45

Na Tatu Mohamed BWAWA la Julius Nyerere (JNHPP) linatarajiwa kuongeza kwa kiasi kikubwa uwezo...

Tanzania kuandika historia leo, Rais Samia kuzindua Bwawa la Julius Nyerere

Na Tatu Mohamed TANZANIA inaandika ukurasa mpya katika historia ya sekta ya nishati leo...