ZOEZI LA UVUTAJI NYAYA AWAMU YA PILI ENEO LA KIKOMBO NA MKONZE KATIKA MRADI WA CHALINZE–DODOMA KUANZA KESHO

📌TANESCO yasema baadhi ya Mikoa ya Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kusini Magharibi na Kanda ya ziwa kupata umeme kwa ratiba maalumu

📌Lengo ni kumpisha Mkandarasi kuendelea na utekelezaji wa Mradi huo wa kusafirisha umeme Msongo wa Kilovolti 400 ambao uko mbioni kukamilika

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limewakumbusha wananchi kuwa, kuanzia Agosti 11 hadi 17, 2026, mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 Chalinze–Dodoma ataendelea na zoezi la uvutaji wa nyaya kwa awamu ya pili katika eneo la Kikombo na Mkonze, Dodoma, katika mradi huo ambao uko mbioni kukamilika.

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Bi. Irene Gowelle, amesema hatua hiyo imekuja baada ya awamu ya kwanza ya uvutaji wa nyaya kutoka Chalinze hadi Mkambarani, Morogoro, kufanyika kwa mafanikio makubwa.

Amesema kutokana na kazi hiyo, baadhi ya mikoa itapata umeme kwa ratiba maalumu. Mikoa hiyo ni ile inayopatikana katika Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kusini Magharibi na Kanda ya Ziwa. Aidha, amesisitiza kuwa mikoa ambayo haitaathirika katika kanda hizo ni pamoja na Morogoro na Tanga.

Ameongeza kuwa mikoa inayotoka katika Kanda hizo zitakosa umeme kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni. Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kukamilisha mradi huo, ambao unatarajiwa kuwa na mchango chanya katika kuimarisha mfumo wa usafirishaji na upatikanaji wa umeme nchini.

‘’Hii ni awamu ya pili ya zoezi la uvutaji wa nyaya katika eneo la Kikombo na Mkonze Mkoani Dodoma, niwaondoe hofu wananchi kwamba tutaendelea kutoa ratiba za upatikanaji wa umeme kupitia mitandao yake ya kijamii, ili kuwawezesha wananchi kupanga shughuli zao kulingana na ratiba hiyo’’alisisitiza Bi. Gowelle.

Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma unatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026. Kukamilika kwake kutaongeza uwezo wa mfumo wa usafirishaji wa umeme nchini na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme yenye ubora na uhakika kwa wananchi.

spot_img

Latest articles

SOKO BUBU LA MADINI LAGUNDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini ▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko ▪️Waziri Mavunde...

Msajili wa Hazina ateta na Rais wa Benki ya Biashara na Maendeleo

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais...

MHANDISI SWEDI: NANENANE NI FURSA YA KUIMARISHA SEKTA YA MADINI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Aziza Swedi, amesema...

Zimamoto yatoa elimu ya uokoaji, yakazia hatua za awali wakati wa majanga

Na Mwandishi Wetu, Dodoma JESHI la Zimamoto na Uokoaji limeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu...

More like this

SOKO BUBU LA MADINI LAGUNDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini ▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko ▪️Waziri Mavunde...

Msajili wa Hazina ateta na Rais wa Benki ya Biashara na Maendeleo

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais...

MHANDISI SWEDI: NANENANE NI FURSA YA KUIMARISHA SEKTA YA MADINI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Aziza Swedi, amesema...