DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imetangaza kusitishwa kwa huduma ya maji kwa takribani saa 12 katika maeneo ya Dar es Salaam na Pwani, kesho Alhamisi, Septemba 10, 2026.

‎Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano DAWASA, Bi Everlasting Lyaro amesema huduma itakatika kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni, kutokana na matengenezo kinga ya miundombinu ya maji katika Mtambo wa Ruvu Juu uliopo Kibaha, yanayolenga kujiandaa kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua kubwa zinazotarajiwa.

Amesema maeneo yatakayoathirika kutokana na matengenezo haya ni pamoja na Ruvu Darajani, Ruvu JKT, Vigwaza, Mlandizi, Mbwawa, Soga, Mwendapole, Tanita, Kwa Mathias, Picha ya Ndege, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Malamba Mawili, Saranga, Mbezi, Ubungo, Kimara, Tabata, Segerea, Kinyerezi, Kisukuru, Bonyokwa, Ukonga, Uwanja wa Ndege, Kiwalani, Vingunguti, Gongo la Mboto, Pugu na Kisarawe.

Mamlaka imewataka Wananchi wa maeneo hayo kuhifadhi maji ya kutosha kwa matumizi muhimu wakati wa matengenezo, huku ikiomba ushirikiano wao ili kazi hiyo ikamilike kwa ufanisi.


spot_img

Latest articles

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...

SAPP kufungua Fursa kwa Tanzania Kuwa Kitovu cha Biashara ya Umeme Kusini mwa Afrika

📌Nchi 18 Zakutana Zanzibar kujadili usalama wa nishati ya umeme kusini mwa Afrika 📌Kuuza au...

WATAHINIWA 1.16 MILIONI KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 Tanzania Bara wanatarajiwa...

More like this

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...

SAPP kufungua Fursa kwa Tanzania Kuwa Kitovu cha Biashara ya Umeme Kusini mwa Afrika

📌Nchi 18 Zakutana Zanzibar kujadili usalama wa nishati ya umeme kusini mwa Afrika 📌Kuuza au...