Na Mwandishi Wetu
RAIS Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa matukio ya ghasia yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, hatua hiyo ni kutekeleza mapendekezo ya Tume ya Rais iliyochunguza matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea kipindi cha uchaguzi huo, kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.
Walioteuliwa kuunda Tume hiyo ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Shabani Ally Lila ameteuliwa kuwa Kamishna na Mwenyekiti wa Tume.
Wengine walioteuliwa ni Gad Mjemmas, Awadh Mohamed Bawazir pamoja na Aishieli Sumari ambao wote ni Majaji Wastaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania.



