Kamati ya uratibu ya Mradi wa SOFF yakutana jijini Dodoma

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), walifanya kikao kazi cha tano cha Kamati ya Uratibu wa Mradi wa SOFF (Systematic Observations Financing Facilit) katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.

Kikao hicho kiliwakutanisha wataalamu muhimu ili kupitia maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa SOFF na kujadili vipaumbele vya kimkakati kwa mwaka 2026, vinavyolenga kuhakikisha ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za mradi.

Majadiliano yalijikita katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mwaka 2026, ufuatiliaji na tathmini ya mradi, pamoja na shughuli za mawasiliano na uhamasishaji zilizopangwa kwa mwaka 2026.

Kamati pia ilipitia maamuzi na maelekezo kutoka kikao cha Tatu cha Kamati Tendaji ya Mradi wa SOFF kilihofanyika Aprili 2026.

Wakizungumza katika ufunguzi, Wenyeviti wenza wa kamati hiyo, Dkt. Paschal Waniha kutoka TMA na Dkt.Abbas Kitogo kutoka UNDP, walisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha utekelezaji unafanyika kwa wakati katika shughuli zote zilizopangwa za mradi wa SOFF Tanzania.

Aidha,kikao kilihitimishwa kwa wajumbe kutoa dhamira ya pamoja ya kuimarisha uratibu, kuharakisha utekelezaji wa shughuli zilizopangwa, na kuongeza ufanisi wa jumla wa mradi wa SOFF nchini Tanzania.

spot_img

Latest articles

ACT Wazalendo Nungwu yafanya mkutano Mkuu wa Kikatiba, Wajumbe zaidi ya 140 washiriki

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa Chama cha...

Tanesco yawataka wananchi kutofanya shughuli za kiuchumi

📌Ni katika zoezi la ukaguzi wa miundombinu ya umeme Tegeta na Mabibo 📌Yatoa rai kwa...

Rejoinder: Tanga Is Still the Strategic Bet, and Tanzania Can Win It

By Peter C. Mhando, PhD Amani Mrope is right: capital has memory. But memory cuts...

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

More like this

ACT Wazalendo Nungwu yafanya mkutano Mkuu wa Kikatiba, Wajumbe zaidi ya 140 washiriki

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa Chama cha...

Tanesco yawataka wananchi kutofanya shughuli za kiuchumi

📌Ni katika zoezi la ukaguzi wa miundombinu ya umeme Tegeta na Mabibo 📌Yatoa rai kwa...

Rejoinder: Tanga Is Still the Strategic Bet, and Tanzania Can Win It

By Peter C. Mhando, PhD Amani Mrope is right: capital has memory. But memory cuts...