Na Mwandishi Wetu
WAKURUGENZI wa Kampuni ya Media Brains wameapishwa wameteuliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) kuwa miongoni mwa majaji wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania 2026 (EJAT).
Walioteuliwa ni Jesse Kwayu, Absalom Kibanda na Neville Meena, ni miongoni mwa majaji 12 wa tuzo hizo waliapishwa wameapishwa leo Aprili 13, 2026 jijini Dar es Salaam na Wakili Ally Kileo,
Wengine wanaunda jopo hilo la majaji ni Joyce Shebe, Beatrice Bandawe, Rashid Kejo, Dk. Egbert Mkoko, Hassan Mhelela, Mwanzo Millinga, Sauli Gilliard, Shifaa Said Hassan na Aisha Dachi.
Akizungumzia uteuzi huo, Katibu Mtendaji wa MCT, Ernest Sungura amesema mfumo huo mpya wa majaji ni mabadiliko makubwa kutoka kwenye tathmini za kizamani zilizokuwa zikizingatia zaidi ubora wa uandishi na uhariri pekee.
Sungura amebainisha kuwa wakati mchujo wa awali wataendelea kuzingatia misingi mikuu ya uandishi wa habari ikiwamo usawa, uwiano, uwazi, na usahihi hatua ya fainali sasa itahitaji uthibitisho wa matokeo ya kazi hiyo katika jamii.
“Kwa sasa tunaenda na mfumo mpya “Uhakiki wa nyanjani” (Field verification) unaolenga kuimarisha uaminifu wa vyombo vya habari kwa jamii,” amesema Sungura.


