CRDB yaandika historia, yapata faida ya Trilioni 1

Na Mwandishi wetu

BENKI ya CRDB imepata faida ya Sh trilioni moja kabla ya kodi katika Kipindi cha mwaka 2025 ikiwa ni mara ya kwanza kuandika historia hiyo.

Akizungumza wakati wa sherehe za utoaji tuzo za CEO AWARDS zilizofanyika katika Ukumbi wa Super Dome Masaki jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt Abdulmajid Nsekela, amesema hatua hiyo imeifanya benki izidi kutambuliwa ndani na nje ya nchi na kutunukiwa tuzo nyingi kama vile kutambuliwa kuwa benki bora Tanzania, benki bora kwa wateja wadogo na wa Kati ambazo zinaenda sambamba na ubora wa wafanyakazi walionao.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Wakurugenzi CRDB, Dkt Ally Laay, amesema anajivunia utendaji uliotukuka wa Dkt Nsekela kutokana na mafanikio iliyopata benki hiyo kwa kipindi kifupi tangu achukue nafasi hiyo.

Amesema wakati Dkt Nsekela anachukua nafasi ya CEO hisa ilikiwa Sh 95 lakini hivi sasa imepanda na kufikia Sh 3,150 akisema hatua hiyo imetengeneza matajiri wengi kwa kupanda kwa bei ya hisa.

Tuzo hizo za heshima zinalenga kuwatambua wafanyakazi na idara zilizofanya vizuri na kuwapa motisha kuonyesha benki yao inawathamini.

spot_img

Latest articles

TUNATAMANI KUWA MABALOZI WA VIPIMO – WANAFUNZI MWANZA

Na WMA - Mwanza WANAFUNZI kutoka shule mbalimbali za Msingi na Sekondari jijini Mwanza wameomba...

Msajili wa Hazina ataka mageuzi makubwa TBC

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, ametaka kufanyika kwa mageuzi makubwa...

CRDB YAZINDUA UGHAIBUNI LOAN KUSAIDIA WATANZANIA WALIOPATA AJIRA NJE YA NCHI

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imezindua rasmi huduma ya mkopo ya Ughaibuni yenye...

Ofisi ya Msajili wa Hazina kuimarisha ushirikiano na taasisi za umma za China

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) iko katika hatua za mwisho za...

More like this

TUNATAMANI KUWA MABALOZI WA VIPIMO – WANAFUNZI MWANZA

Na WMA - Mwanza WANAFUNZI kutoka shule mbalimbali za Msingi na Sekondari jijini Mwanza wameomba...

Msajili wa Hazina ataka mageuzi makubwa TBC

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, ametaka kufanyika kwa mageuzi makubwa...

CRDB YAZINDUA UGHAIBUNI LOAN KUSAIDIA WATANZANIA WALIOPATA AJIRA NJE YA NCHI

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imezindua rasmi huduma ya mkopo ya Ughaibuni yenye...