CRDB yaandika historia, yapata faida ya Trilioni 1

Na Mwandishi wetu

BENKI ya CRDB imepata faida ya Sh trilioni moja kabla ya kodi katika Kipindi cha mwaka 2025 ikiwa ni mara ya kwanza kuandika historia hiyo.

Akizungumza wakati wa sherehe za utoaji tuzo za CEO AWARDS zilizofanyika katika Ukumbi wa Super Dome Masaki jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt Abdulmajid Nsekela, amesema hatua hiyo imeifanya benki izidi kutambuliwa ndani na nje ya nchi na kutunukiwa tuzo nyingi kama vile kutambuliwa kuwa benki bora Tanzania, benki bora kwa wateja wadogo na wa Kati ambazo zinaenda sambamba na ubora wa wafanyakazi walionao.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Wakurugenzi CRDB, Dkt Ally Laay, amesema anajivunia utendaji uliotukuka wa Dkt Nsekela kutokana na mafanikio iliyopata benki hiyo kwa kipindi kifupi tangu achukue nafasi hiyo.

Amesema wakati Dkt Nsekela anachukua nafasi ya CEO hisa ilikiwa Sh 95 lakini hivi sasa imepanda na kufikia Sh 3,150 akisema hatua hiyo imetengeneza matajiri wengi kwa kupanda kwa bei ya hisa.

Tuzo hizo za heshima zinalenga kuwatambua wafanyakazi na idara zilizofanya vizuri na kuwapa motisha kuonyesha benki yao inawathamini.

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...