Latra yawaonya wanaopandisha nauli

Na Mwandishi wetu

MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imewataka Wasafirishaji nchini kuwa watulivu na kuepuka kupandisha nauli kiholela kufuatia ongezeko la bei za mafuta ya Dizeli, Petroli na Mafuta ya Taa kwa mwezi Aprili.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 1, 2026, Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, Habibu Suluo amesema mamlaka hiyo inatambua changamoto zinazosababishwa na mabadiliko ya bei ya mafuta, huku akisisitiza kuwa hatua yoyote ya kuongeza nauli lazima ifuate taratibu rasmi zilizowekwa.

“Tunawaomba Wasafirishaji kuwa na subira katika kipindi hiki. Wasipandishe nauli bila kufuata utaratibu rasmi hadi pale tutakapokutana nao na kujadiliana kwa pamoja,” amesema Suluo.

Ameongeza kuwa LATRA imepanga kukutana na Wadau wa Sekta ya Usafirishaji Aprili 8, mwaka huu ili kujadili mustakabali wa nauli za usafiri wa umma na kufikia muafaka utakaolinda maslahi ya pande zote, wakiwemo abiria na watoa huduma.

Amefafanua kuwa, hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa mabadiliko yoyote ya nauli yanazingatia hali halisi ya uchumi na hayawaumizi Wananchi wanaotegemea usafiri wa umma katika shughuli zao za kila siku.

Aidha, wananchi wametakiwa kuripoti vitendo vyovyote vya upandishaji holela wa nauli kwa mamlaka husika hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...