Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu

WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi Kuu Tanzania, timu hiyo itawakosa wachezaji wake muhimu wanaokabiliwa na majeraha akiwamo mshambuliaji Laurindo Dilson ‘Depu’.

 Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea  mchezo huo utakaopigwa kesho saa 10:00 alasiri, katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, Kocha Mkuu wa Yanga Pedro Goncalves  amesema wamekuwa na ratiba ngumu ya michezo mfululizo ukizingatia wametoka kucheza mechi ngumu siku chache zilizopita tofauti na wapinzani wao.

Amesema wanakwenda kukabiliana na timu ambayo imepata muda wa kutosha wa mapumziko na maandalizi lakini wamejipanga kuchukua pointi tatu.

“Pia tumekubwa na idadi kubwa ya majeruhi. Lakini hali hiyo inatoa fursa kwa wachezaji wengine wenye hali nzuri,” amesema.

Uongozi wa Klabu ya Yanga umetoa taarifa ya  kuthibitisha kuwa wachezaji wake wanne wakiwemo  Chadrack Boka, Edmund John pamoja na Ibrahim Abdullah ‘Bacca’ wamepata majeraha na wanatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa.

Wachezaji wengine ni Chadrack Boka ambaye amepata jeraha la enka ya mguu wa kushoto na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili, na Edmund John ambaye amepata jeraha la bega na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili.

spot_img

Latest articles

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

More like this

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...