Menejimenti ya TMDA yajipanga na Dira 2050

Na Mwandishi Wetu

MENEJIMENTI ya TMDA imekutana Morogoro Februari 2 hadi 3, 2026 kujadili rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Mamlaka wa miaka mitano, 2026/27-2030/31 unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050.

Rasimu ya Mpango Mkakati huo ni ya Sita kufuatia kukamilika kwa ufanisi kwa Mpango Mkakati wa Tano.

Mpango Mkakati wa Sita wa TMDA unatarajiwa kuanza kutumika mnamo tarehe 01, Julai, 2026.

Pamoja na mambo mengine, rasimu ya Mpango Mkakati husika inalenga katika kuhakikisha ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa za dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa lengo la kulinda afya ya Jamii.

Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, aliwaeleza wajumbe wa kikao husika kuwa rasimu husika ya Mpango Mkakati inabeba Dira mpya ya TMDA ambayo ni “Kuimarika kwa afya na ustawi wa Watanzania wote kupitia udhibiti bora unaokidhi viwango vya kitaifa”.

Dkt. Fimbo aliongeza kuwa, Dhamira Mpya ya Taasisi itakuwa ” Kulinda Afya ya Jamii kwa kuhakikisha, usalama, ubora na ufanisi wa dawa, vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa zote zinazohusiana na afya”.

Uongozi wa TMDA umekuwa na utamaduni shirikishi katika kujadili mambo makubwa yahusuyo taasisi, ambapo watumishi wote hushirikishwa kupitia ngazi mbalimbali ndani ya Mamlaka kabla ya kuidhinishwa na Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB).

Pamoja na mambo mengine, Mpango Mkakati huu mpya unaweka mwelekeo wa pamoja katika udhibiti, utasaidia katika kupanga matumizi ya rasilimali vizuri na kuboresha uwajibikaji na uwazi.

Mpango Mkakati wa TMDA ni nyaraka muhimu ambayo inaonesha ramani ya safari ya taasisi na ndiyo chombo muhimu cha kuongoza maamuzi na maendeleo ya TMDA.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...