Rais Samia kushiriki mkutano wa WGS 2026

Na Mwandishi Wetu

RAIS Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Februari 2, 2026 kwenda Dubai, Falme za Kiarabu, ambapo anatarajiwa kushiriki katika uzinduzi wa mpango wa Global Africa Investment Summit (GAIS) utakaofanyika kwa pamoja na mkutano wa Dunia wa Serikali (WGS 2026).

Mkutano wa WGS 2026, unaobeba kaulimbiu “kutengeneza serikali zijazo (Shaping Future Governments)”, ni jukwaa la kimataifa linalowakutanisha wakuu wa nchi na serikali, watunga sera, viongozi wa taasisi za kimataifa, sekta binafsi na wawekezaji wakubwa kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Ushiriki wa Rais Samia katika mkutano huo unaweka mkazo katika diplomasia ya uchumi, huku lengo kuu likiwa ni kuoanisha sera za maendeleo ya Tanzania na mwelekeo wa mitaji ya kimataifa na kuharakisha uwekezaji unaochochea ajira na ukuaji wa uchumi.

Sambamba na WGS, Rais Samia atashiriki uzinduzi wa Global Africa Investment Summit (GAIS), jukwaa la kimkakati la uwekezaji lililoanzishwa na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dk Akinwumi Adesina kwa kushirikiana na wadau wa kimataifa.

Mpango wa GAIS ulianzishwa na Dk. Akinwumi Adesina, Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kwa kushirikiana na wadau wa kimataifa, lengo kuu likiwa ni kuunganisha miradi yenye tija barani Afrika na wawekezaji wa kimataifa ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza fursa za ajira.

spot_img

Latest articles

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

More like this

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...