Rais Samia kushiriki mkutano wa WGS 2026

Na Mwandishi Wetu

RAIS Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Februari 2, 2026 kwenda Dubai, Falme za Kiarabu, ambapo anatarajiwa kushiriki katika uzinduzi wa mpango wa Global Africa Investment Summit (GAIS) utakaofanyika kwa pamoja na mkutano wa Dunia wa Serikali (WGS 2026).

Mkutano wa WGS 2026, unaobeba kaulimbiu “kutengeneza serikali zijazo (Shaping Future Governments)”, ni jukwaa la kimataifa linalowakutanisha wakuu wa nchi na serikali, watunga sera, viongozi wa taasisi za kimataifa, sekta binafsi na wawekezaji wakubwa kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Ushiriki wa Rais Samia katika mkutano huo unaweka mkazo katika diplomasia ya uchumi, huku lengo kuu likiwa ni kuoanisha sera za maendeleo ya Tanzania na mwelekeo wa mitaji ya kimataifa na kuharakisha uwekezaji unaochochea ajira na ukuaji wa uchumi.

Sambamba na WGS, Rais Samia atashiriki uzinduzi wa Global Africa Investment Summit (GAIS), jukwaa la kimkakati la uwekezaji lililoanzishwa na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dk Akinwumi Adesina kwa kushirikiana na wadau wa kimataifa.

Mpango wa GAIS ulianzishwa na Dk. Akinwumi Adesina, Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kwa kushirikiana na wadau wa kimataifa, lengo kuu likiwa ni kuunganisha miradi yenye tija barani Afrika na wawekezaji wa kimataifa ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza fursa za ajira.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...