Mzee Mtei kuzikwa Jumamosi Tengeru

Na Mwandishi Wetu


MWASISI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mzee Edwin Mtei anatarajiwa kuzikwa Jumamosi ya Januari 24, 2026 nyumbani kwake Tengeru nje kidogo ya Jiji la Arusha.

Mzee Mtei ambaye pia alikuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), alifariki dunia usiku wa Jumatatu, Januari 19, 2026 jijini Arusha, akiwa na umri wa miaka 94.

Aidha viongozi mbalimbali wamefika nyumbani kwa marehemu akiwemo Mwenyekiti mstaafu wa Chadema Freeman Mbowe ambaye ni msemaji wa familia kwa sasa.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ratiba ya mazishi, Mbowe amesema msiba wa Mzee Mtei ni wa kijamii na unawahusu watu wa makundi mbalimbali ndani na nje ya siasa, kutokana na mchango wake mkubwa katika historia ya Tanzania, hivyo waombolezaji kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kushiriki mazishi hayo.

“Huu ni msiba shirikishi. Kwanza huyu ni senior citizen aliyelitumikia taifa tangu kipindi cha uhuru na hata kabla ya uhuru. Huu si msiba wa mtu mmoja, ni msiba jumuishi unaowahusu wanasiasa na wasio wanasiasa,” amesema Mbowe.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...