Mradi wa Umeme Jua uko mbioni kukamilika- Salome Makamba

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema Mradi wa Umeme unaozalishwa kwa nguvu ya Jua uliopo Kishapu, Mkoani Shinyanga, uko mbioni kukamilika ambapo jumla ya megawati 50 zinatarajiwa kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ili kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Shinyanga na mikoa jirani.

Salome ameyasema hayo Januari 9, 2026, wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya umeme mkoani Shinyanga, ukiwemo Mradi wa Umeme wa Jua Kishapu, Mradi wa upanuzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Ibadakuli pamoja na Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Ibadakuli kwenda Mkoa wa Simiyu.

Amesema kuwa hadi sasa mradi wa Umeme wa Jua Kishapu umefikia zaidi ya asilimia 89 ya utekelezaji wake na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu, ikiwa ni jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali za kuhakikisha nchi inakuwa na umeme wa kutosha kwa ajili ya kukuza fursa kiuchumi na maendeleo endelevu.

“Mradi huu umefikia zaidi ya asilimia 89 ya utekelezaji wake, na tunatarajia kwamba ifikapo mwishoni mwa mwezi huu tutaingiza megawati 50 kwenye Gridi ya Taifa. Huu ni muendelezo wa juhudi za Serikali kuhakikisha Tanzania inakuwa na umeme wa kutosha na mtandao imara wa kusafirisha na kusambaza umeme,” alisisitiza Salome.

Akizungumza katika Mradi wa Upanuzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Ibadakuli, ambao umefikia asilimia 44.32 , Naibu Waziri huyo wa Nishati amesema mradi huo una umuhimu mkubwa kwa kuwa utakuwa na uwezo wa kupeleka umeme katika reli ya kisasa ya SGR pamoja na nchi jirani za Kenya na Uganda.

“Tunamshukuru na kumpongeza Rais kwa kutoa fedha kwa ajili ya upanuzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Ibadakuli. Kwetu sisi ni heshima kubwa kwa kuwa kituo hiki kitahudumia mradi mkubwa wa kimkakati wa SGR, sambamba na kupeleka umeme katika nchi jirani za Kenya na Uganda,” alifafanua Naibu Waziri Salome.

Akizungumzia Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Ibadakuli hadi Simiyu, Kaimu Mkurugenzi wa Miradi TANESCO, Mhandisi Frank Mashalo, amesema lengo la mradi huo ni kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Simiyu na mikoa Jirani ambapo hadi sasa mradi umefikia asilimia 53 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni mwaka huu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Peter Masindi, amesema kukamilika kwa mradi huo kutachochea shughuli za uzalishaji na uchumi kwa wananchi wa Kishapu, wengi wao wanajishughulisha na kilimo cha pamba, ambacho kinahitaji nishati ya umeme kwa ajili ya uzalishaji.

Mradi wa Umeme wa Jua Kishapu unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 323 kwa awamu zote mbili. Mradi huo ulianza rasmi mwezi Desemba 2023 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Januari 2026.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...