Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Familia yaondoa vitu nyumbani kwa Polepole

Na Mwandishi Wetu

FAMILIA ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, leo Jumanne, Januari 6, 2026, imefika katika nyumba aliyokuwa akiishi eneo la Ununio jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kukusanya mali zake, pamoja na kufanya maombi kwenye nyumba aliyokuwa akiishi.

Ndugu hao wakiongozwa na mama mzazi wa Humphrey Polepole, Mama Anna Marry Polepole na mdogo wake Godfrey Polepole, wamesema wataendelea kumuombea ndugu yao na kuisihi jamii kuendelea kushirikiana na vyombo husika pale taarifa zozote zitakapopatikana

Akizungumza na waandishi wa habari, Mama wa Polepole ameeleza kuwa wamekwenda kutoa vitu katika nyumba hiyo aliyokuwa amepanda mwanaye kwa sababu hakuna anayeweza kulipa kodi.

Amesisitiza kuwa anaomba waliomchukua mtoto wake wamrudishe akiwa mzima  na ikiwa ana makosa aliyofanya  ashtakiwe kama wengine.

Polepole, ambaye aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini alidaiwa kutekwa na watu wasiojulikana miezi mitatu iliyopita na hadi sasa hatima yake ikiwa bado haijulikani rasmi.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...