Chongolo akutana na wawekezaji  kutoka China

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, amekutana na wawekezaji kutoka nchini China  na kujadili uwekezaji katika Sekta ya Kilimo hususan kuongeza uzalishaji wa mazao, thamani na kuleta teknolojia za kisasa zitakazoleta tija kwa wakulima.

Mkutano huo umefanyika Januari 5, 2026, jijini Dar es Salaam ambapo wawekezaji hao wameonesha nia ya kuwekeza katika mazao ya kimkakati, likiwemo zao la korosho, kuanzia uzalishaji hadi uongezaji wa thamani wa zao hilo.  

Akieleza zaidi kuhusu majadiliano yao, Waziri Chongolo amesema kuwa wawekezaji pia wamehamasishwa kuwekeza katika uzalishaji wa mafuta ya korosho, methanol na bidhaa nyingine.  Eneo lingine ni zao la Soya kwa ajili ya chakula cha binadamu na mifugo, hatua itakayosaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza upatikanaji wa malighafi kwa viwanda vya ndani.

Majadiliano hayo pia yalilenga kilimo cha vitunguu na uwekezaji katika mashine zinazorahisisha utengenezaji wa matuta kwa wakulima wa mpunga ili kupunguza muda na gharama za kazi shambani. 

Kwa niaba ya timu ya wawekezaji, Bw. Li Qingyu amesema uwekezaji wao utalenga kuongeza uzalishaji, kuhamisha teknolojia ya kisasa kwa wakulima, kuongeza ujuzi na kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuimarisha uongezaji wa thamani wa mazao ya kilimo. 

Waziri Chongolo amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje waliolenga kuongeza thamani ya mazao na kuimarisha teknolojia ya kisasa katika kilimo.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...