Chongolo akutana na wawekezaji  kutoka China

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, amekutana na wawekezaji kutoka nchini China  na kujadili uwekezaji katika Sekta ya Kilimo hususan kuongeza uzalishaji wa mazao, thamani na kuleta teknolojia za kisasa zitakazoleta tija kwa wakulima.

Mkutano huo umefanyika Januari 5, 2026, jijini Dar es Salaam ambapo wawekezaji hao wameonesha nia ya kuwekeza katika mazao ya kimkakati, likiwemo zao la korosho, kuanzia uzalishaji hadi uongezaji wa thamani wa zao hilo.  

Akieleza zaidi kuhusu majadiliano yao, Waziri Chongolo amesema kuwa wawekezaji pia wamehamasishwa kuwekeza katika uzalishaji wa mafuta ya korosho, methanol na bidhaa nyingine.  Eneo lingine ni zao la Soya kwa ajili ya chakula cha binadamu na mifugo, hatua itakayosaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza upatikanaji wa malighafi kwa viwanda vya ndani.

Majadiliano hayo pia yalilenga kilimo cha vitunguu na uwekezaji katika mashine zinazorahisisha utengenezaji wa matuta kwa wakulima wa mpunga ili kupunguza muda na gharama za kazi shambani. 

Kwa niaba ya timu ya wawekezaji, Bw. Li Qingyu amesema uwekezaji wao utalenga kuongeza uzalishaji, kuhamisha teknolojia ya kisasa kwa wakulima, kuongeza ujuzi na kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuimarisha uongezaji wa thamani wa mazao ya kilimo. 

Waziri Chongolo amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje waliolenga kuongeza thamani ya mazao na kuimarisha teknolojia ya kisasa katika kilimo.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...