Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi

BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake la kesho dhidi ya Mnaigeria, Stanley Eribo litakuwa la kisasi, huku Hamad Furahisha akitaka kuweka rekodi ya kumchapa Mmalawi Hanock Phiri.

Mabondia hao wanatarajia kupanda ulingoni kesho Desemba 26, kuzichapa katika pambano lililopewa jina la Boxing On Boxing Day kwenye Ukumbi wa Warehouse, jijjni Dar es Salaam.

Akizungumzia mchezo huo, Mwakinyo amesema kuwa hadi kufikia hatua ya kupima uzito na kila mtu afya yake ipo sawa, hakuna sababu ya kuzuia pambano hilo lisipigwe.

“Kutokana na afya za watu wote hapa ni nzuri, nafikiri hakuna sababu ya kufanya pambano lisipigwe. Mimi sina mengi ya kuongea kisasi kitafanywa,” ametamba Mwakinyo.

Naye Furahisha amesema mpinzani wake anatamba kwa kuwa amewapiga baadhi ya mabondia hapa nchini lakini ajue safari hii atakutana na kitu tofauti na kipigo kinamhusu.

Amesema amesindikizwa na watu wengi kwenda kupima uzito akiwamo diwani, wote wakiwa na imani naye, hivyo hatawaangusha watanzania.

Kwa upande wake Mratibu wa matukio wa Peak Time ambao ni waandaaji wa mapambano yako, Bakari Hatibu, amesema maandalizi yote yamekamilika na mabondia wote waliotakiwa wamefika.

Mapambano mengine Hassan Ndonga atazichapa na Ismail Boyka, Ally Ngwando vs Mussa Makuka
Issa Simba (Kahama) vs Wilson Phiri (Malawi), Debora Mwenda vs Mariam Dick (Malawi) na Leila Machi vs Hidaya Zahoro.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...