Watanzania waaswa kudumisha amani, Umoja na mshikamano

Na Mwandishi Wetu

KATIKA kuadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika, Watanzania wametakiwa kukumbuka siku hiyo kwa misingi ya haki, amani, mshikamano na umoja wa kitaifa, huku wakiepuka mivutano yoyote inayoweza kugawanya taifa, ikiwemo migawanyiko ya kidini, kikabila au kisiasa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Everlasting Legal Aid Foundation, Dkt. Khamis Masoud, amesema kuwa kumbukizi ya uhuru inapaswa kuwa fursa ya kuimarisha mshikamano na kuwaunganisha Watanzania wote bila kujali tofauti zao.

Dkt. Masoud amesema ni muhimu viongozi wa dini na serikali kuungana katika kuhubiri amani, heshima na ustahimilivu, kwa kuwa wao ni nguzo muhimu katika kuunganisha jamii.

“Ni muhimu viongozi wa dini kutazama namna bora ya kuwaleta wananchi pamoja kuhusu amani badala ya kufanya mambo yanayoweza kugawanya taifa kwa mitazamo ya kidini,” amesema Dkt. Masoud.

Aidha, amesisitiza kuwa viongozi wa serikali wanapaswa kuwa wazalendo na wenye uthubutu wa kuchukua maamuzi magumu kwa maslahi ya taifa.

Ameongeza kuwa hata pale ambapo ni lazima, viongozi hao wanapaswa kuwa tayari kung’atuka madarakani ili kulinda amani, mshikamano na haki nchini.

Mbali na hayo, Dkt. Masoud amebainisha umuhimu wa kuimarisha diplomasia na mahusiano ya kimataifa, akieleza kuwa Tanzania inahitaji uhusiano mzuri na mataifa mbalimbali ili kuendeleza maendeleo na uchumi wa nchi.

Ameitaka serikali kuendelea kumuunga mkono Rais katika utekelezaji wa mikakati ya kidiplomasia yenye manufaa kwa taifa.

Itakumbukwa kuwa kwa mwaka 2025, serikali iliahirisha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika, na kuelekeza fedha zilizokuwa zimepangwa kutumika katika sherehe hizo kufadhili ukarabati wa miundombinu iliyoathiriwa na vurugu za uchaguzi mkuu zilizotokea Oktoba 29, 2025.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...