Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amesema yuko tayari kuitwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ili kujibu tuhuma zinazomhusisha na umiliki wa vituo vya mafuta vya Lake Oil.

Amesema hayo alipokuwa akizungumza na watumishi wa wizara hiyo Novemba 26, 2025, akibainisha kuwa ni muhimu taarifa za watumishi wa umma kuwa wazi.

Amesisitiza kuwa pale panapojitokeza sintofahamu, viongozi wanapaswa kuhojiwa na taarifa kuwekwa hadharani ili wananchi wapate ukweli.

“Malalamiko juu ya viongozi yamekuwa mengi sana; haijulikani lipi ni kweli na lipi si kweli,” amesema.

Akitoa mfano, Ridhiwani amesema maandamano yaliyotokea hivi karibuni yalihusisha malalamiko kuhusu maadili ya viongozi, ambapo ilidaiwa kuwa vituo vya mafuta vinavyojulikana kama Lake Oil vinamilikiwa naye.

“Kuna mtu mmoja anaitwa Ali Edha; ana vituo vya mafuta vinavyoitwa Lake Oil, lakini vimechomwa kwa madai kuwa ni vya Ridhiwani,” amesema.

Ridhiwani aliitaka tume hiyo kumuita bila hofu ili kumhoji, huku akipendekeza uchunguzi ufanyike kwanza na baada ya kukamilika waandaliwe waandishi wa habari. Pia alishauri tume iombe ushahidi wa ziada kutoka kwa umma ili kuweka ukweli hadharani.

spot_img

Latest articles

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

Dk. Nchimbi: Serikali imejipanga kuimarisha sekta ya uchukuzi

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi amesema serikali imejizatiti kuhakikisha...

More like this

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...