Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na heshima kwa familia zilizopoteza wapendwa wao, akipinga namna ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakichapisha taarifa au picha mtandaoni kana kwamba vifo ni jambo la kusherehekewa.

Amesema hayo wakati akijibu maswali aliyoulizwa  kwenye mkutano na wahariri wa vyombo vya habari ya kutaka kujua idadi ya vifo vilivyotokea Oktoba 29, 2025  kutokana na maandamano yaliyofanyika na kusababisha vurugu.

“Tunaongelea maisha ya watu, tunaongelea watu waliopoteza wapendwa wao. Mtu amepoteza ndugu yake halafu wewe unaposti kama hafla,” amesema Waziri Mkuu, akionyesha masikitiko yake juu ya tabia ya kutafuta umaarufu kupitia misiba.

“Katika mazingira ambayo mtu amepoteza mpendwa wake mnataka tuanze kuhesabu kama majengo, magari au mafanikio? Mwingine anataja idadi licha ya kwamba hayupo hapa,” ameeleza.

Aidha Dk. Mwigulu ametaja  vitu vilivyoharibiwa  kutokana na vurugu hizo kuwa ni magari 1,642 ya watu binafsi yaliharibiwa, baadhi yakiteketezwa kwa moto, vituo vya mafuta 672 na bodaboda 2,268.

Amesisitiza umuhimu wa kuzingatia utulivu na amani, akibainisha kuwa Watanzania wanapaswa kuepuka fujo zinazoweza kuharibu maisha na ustawi wa kila mmoja.

Ametoa wito kwa Watanzania kuwa makini na makundi ya watu wenye nia ya kuichafua na kuiharibu Tanzania na wakatae kutumiwa kufanya uovu.

“Kila mmoja alibebe jambo hili kwa ukubwa, hawatupendi, wanaangalia rasilimali zetu, nchi yetu sio masikini, kuna watu wanamezea mate rasilimali zetu, ninawahakikishia kuwa tutailinda Tanzania na Rasilimali zake kwa gharama yoyote ile,”

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...