Na Mwandishi Wetu
MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi wa Kiti cha Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ambapo kwa ushindi huo anaenda kuwa Spika wa tisa wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Zungu ameibuka mshindi na kutangazwa hii leo Novemba 11, 2025 kwa Kupata Kura 378 dhidi ya wapinzani wake Veronica Charles Tyeah ambaye hajapata kura kutoka chama cha NFA, Anitha Alfan aliyepata kura moja kutoka chama cha NLD, Ndoge Said Ndonge aliyepata Kura moja kutoka chama cha AAFP pamoja na Amin Alfred Yango ambaye hajapata kura kutoka chama cha ADC.
Zungu amekuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 20 ambapo aliingia bungeni rasmi mwaka 2005.
Kwa kipindi hicho amekuwa Mwenyekiti wa Bunge 2012-2021 na Naibu Spika 2022 mpaka 2025.


