Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu imeahirishwa leo Oktoba 24 hadi Novemba 3, 2025,.

Kesi hiyo iliyoanza kusikilizwa mfululizo tangu Oktoba 6, 2025 imeahirishwa baada ya upande wa Jamhuri kuomba kuahirisha shauri hilo ili kupisha uchaguzi mkuu ambao upo kwa mujibu wa Katiba.

Awali, mshitakiwa Tundu Lissu, aliiomba Mahakama kutoahiriahwa kwa kesi hiyo na kama Mahakama itakubali ombi la upande wa Jamhuri basi yeye apewe dhamana kwa mujibu wa kifungu  302(3) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA), hadi tarehe iliyopangwa kwenye ratiba ya usikilizaji wa kesi hiyo.

Lissu aliwasilisha ombi hilo leo Ijumaa, Oktoba 24, 2025, mara baada ya Jamhuri kuiomba Mahakama kuahirisha usikilizwaji wa kesi hiyo hadi Novemba 3, 2025, kwa maelezo kuwa mashahidi waliopangwa kutoa ushahidi wao leo wanahusiana na vielelezo vilivyokataliwa wiki hii.

Baada ya kusikiliza ombi la pande zote mbili, Jopo la majaji likiongozwa na Dustan Nduguru limekuja na maamuzi ya kuahirisha kesi hiyo huku wakisema ombi la mshitakiwa kuomba dhamana haliwezekani kwani kesi inayomkabili (Uhaini), haina dhamana.

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...