Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi

Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, klabu ya Simba imetamba kuwa ni kati ya timu tatu Afrika zenye uhakika wa kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo Oktoba 21,2025 na Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ahmed Ally wakati akizungumza na waandishi kuelekea mchezo wao wa marudiano na  Nsingizini inayotokea Eswatini,  wakisaka tiketi ya kutinga hatua ya makundi. Mechi hiyo itachezwa Jumapili hii Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Ameeleza kuwa wana sababu zote za kuonyesha utofauti kwa kuwa ndiyo timu pekee kutoka Tanzania iliyopata ushindi ugenini katika michezo ya mkondo wa kwanza raundi ya pili Ligi ya Mabingwa Afrika. “Afrika hii timu zenye uhakika wa kucheza makundi mara saba mfululizo ni Al Ahly na Mamelodi na sisi tunaongezeka hapo.

“Tulikuwa tunapiga kelele kwamba Simba yetu hatuelewi inavyocheza lakini sasa imerejea. Simba ya kutisha imerejea, Simba ya kushambulia muda wote imerejea sasa unabaki nyumbani kufanya nini. Na haya sio maneno ya kutoka usingizi, haya ni maneno ya kuona inacheza na pale mwalimu anasema uwanja ulikuwa mdogo. Sasa uwanja wa Mkapa anakwenda kwenye uwanja mkubwa, njoo Uwanja wa Mkapa uone Simba ikifanya balaa zito, amejinasibu Ahmed.

Amesema mchezo huo pia itakuwa ni nafasi pekee kwa mashabiki kuona  uhalisia wa kocha wao mpya  Dimitar Pantev ambaye licha ya ushindi lakini alisema bado hajaridhishwa na kiwango cha timu yake.

spot_img

Latest articles

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

More like this

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...