Bulugu awahamasisha vijana wa Mlowo kuichagua CCM

Na Mwandishi Wetu

KATIBU Msaidizi Mkuu Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa CCM, Bulugu Magege, leo tarehe 30/09/2025 amekutana na vijana wa Kata ya Mlowo na kuwasisitiza kuhakikisha kura zao zote wanampa Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wa CCM katika ngazi zote.

Katika mazungumzo hayo, Bulugu aliwaeleza vijana kuwa Ilani ya CCM imewapa kipaumbele kikubwa vijana ikiwemo mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri, ajira, elimu bora na uwezeshaji kiuchumi.

Alisisitiza kuwa Dkt. Samia ni Rais mwenye upendo mkubwa kwa vijana, anayetamani kuwaona wakibadilisha maisha yao kupitia fursa alizozileta.

Bulugu aliambatana na Haji Shabani Mwalimu, Katibu wa UVCCM Wilaya ya Mbozi na Noel Donald Mkwemba, Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Mkoa wa Songwe.

Vijana wa Mlowo walimhakikishia kuwa wako tayari kuhakikisha CCM inapata ushindi wa kishindo ifikapo Oktoba 29, 2025.

spot_img

Latest articles

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Msajili wa Hazina, Fitch Ratings watathmini mageuzi ya taasisi za umma

Na Mwandishi wa OTR OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) Jumanne, Agosti 11, 2026, ilifanya...

More like this

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...