Yanga yakiri vita ya kupambana na jezi feki ngumu

Na Winfrida Mtoi, The Media Brains

UONGOZI wa Klabu ya Yanga umekiri kuwa vita ya kudhibiti jezi feki ni ngumu pamoja na jitihada wanazofanya na kutumia mbinu nyingi lakini imeshindikana, walichofanikiwa ni kupunguza madhara na si kukomesha suala hilo.

Hayo yamezungumzwa na Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ali Kamwe leo Septemba 26, 2025 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa jezi mpya toleo la pili ya timu hiyo.

“Vita ya jezi feki sio vita nyepesi, ni vita ngumu mmno, ni vita nzito kupambana nayo, tumetumia mbinu nyingi, tulichofanikiwa ni kupunguza madhara lakini hatujafanikiwa kukomesha tatizo hilo.

Jezi mpya ya Yanga iliyozinduliwa leo

“Sisi tumezindua jezi hivi karibuni na mzigo wetu tulioleta msimu huu umeisha, lakini cha ajabu bado tunaendelea kupewa taarifa kuwa mizigo mikubwa ya jezi bado inaendelea kuingia nchini. Ila uongozi wa Yanga umekuja mpango wa kukomesha hili mwaka huu. Naamini njia tuliyokuja nayo hii itakuwa ni komesha,” amesema Kamwe.

Ameeleza kuwa wamedhamiria kupambana na hata toleo hilo jipya ni moja ya suluhisho kwa kuwa hawawezi kuona klabu inazidi kupoteza mapato na kuwanufaisha wengine.

Hivi karibuni uongozi wa Klabu ya Simba nao ulitoa taarifa za uwepo wa jezi feki zinazouzwa katika mikoa mbalimbali kama vile Morogoro, Singida, Geita na Mwanza.

Mwaka 2023 Ofisa Habari wa Yanga, Kamwe  aliongoza zoezi la kukamata jezi feki za Yanga na Simba kwenye godauni moja maeneo ya Mbozi Road, Temeke, Dar Es Salaam zilizokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya sh. 10 bilioni.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...