Mahakama Kuu yaruhusu ACT Wazalendo, Mpina kufungua Shauri kupinga maamuzi ya Msajili

Na Mwandishi Wetu

MAHAMAMA Kuu ya Tanzania (Masjala Kuu Dodoma) imetoa kibali kwa Chama cha ACT Wazalendo na Luhaga Mpina kufungua shauri la kupinga maamuzi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuondoa jina la Mpina.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na kusainiwa leo Septemba 26, 2025 na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Mahakama hiyo chini ya Jaji Wilbert Chuma imeridhia maombi hayo baada ya kutimiza vigezo vyote vinavyohitajika kisheria pamoja na misingi iliyowekwa na maamuzi ya awali ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania.

ACT Wazalendo na Luhaga Mpina wana siku 14 kuanzia leo za kuwasilisha rasmi maombi ya kufutwa kwa maamuzi hayo ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha, chama cha ACT Wazalendo kimeendelea na shauri la Kikatiba nambari 24027 dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Shauri hilo litasikilizwa Septemba 29, 2025 mbele ya majaji watatu ambao ni Jaji Frederick Manyanda, Jaji Sylvester Kainda na Jaji Abdallah Gonzi.

Itakumbukwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliwasilisha mapingamizi wakitaka maombi hayo yatupiliwe mbali kwa hoja kwamba yanapingana na misingi ya kisheria.

Hata hivyo, Mahakama iliona mapingamizi hayo hayana msingi na kuyatupilia mbali.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...