Kocha Simba aaga, atangazwa Raja Casablanca

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids ameaga rasmi wadau na mashabiki wa klabu hiyo na tayari ametangazwa klabu yake ya zamani ya Raja Casablanca ya nchini Morocco kukinoa kikosi hicho.

Raja Casablanca leo Septemba 22, 2025 imetoa taarifa ya mabadiliko ya benchi lake la ufundi na kumtangaza Fadlu ambaye aliwahi kutumika kama kocha msaidizi, kuwa Kocha Mkuu.

Kocha huyo hakuonekana wakati Simba ikirudi kutoka Botswana ilipokwenda mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United.

Fadlu aliyedumu Simba kwa kipindi cha mwaka mmoja na miezi miwili, ameaga muda mfupi baada ya kusambaa kwa tetesi kuwa kocha huyo ameachana na timu hiyo, licha ya uongozi wa Simba kushindwa kutoa  taarifa rasmi hadi sasa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Fadlu ameandika walaka wa kuaga Simba unaosema: “Ni kwa moyo mzito naiaga Simba. Tangu nilipowasili, nilihisi shauku ya klabu hii kubwa na upendo wa mashabiki wake wa ajabu. Kwa pamoja tulipigana, kusherehekea, na kuimarika kupitia kila ushindi na kila changamoto.

Shukrani zangu za dhati kwa Rais Mo Dewji kwa uongozi wake wa kutia moyo, maono, na msaada wake wa kila mara.

Kwa wachezaji: endelea kupigana, endelea kuamini, na endelea kuinua beji kwa heshima. Kwa wafanyikazi na wasimamizi: asante kwa uaminifu wako na kujitolea bila kuchoka nyuma ya pazia.

Kwa mashabiki wa Simba: Wewe ndiye mapigo ya moyo wa klabu hii. Sauti zako, nyimbo zako, shauku yako isiyoyumba zitasikika katika kumbukumbu yangu. Asante kwa kukaribisha familia yangu kama yako.

Simba daima itakuwa sehemu yangu, na ninaitakia klabu mafanikio, mafanikio na vikombe mbeleni. Asanteni Sana, forever Nguvu Moja ,”

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...