Mkurugenzi Mkuu Dawasa Mtaa kwa Mtaa kukagua huduma za maji

Na Mwandishi Wetu

AFISA Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Mkama Bwire amefanya ziara ya kikazi kukagua hali ya upatikanaji wa maji katika maeneo ya Ubungo, Mburahati, Magomeni, Saranga na Kinyerezi.

Ziara hiyo ililenga kujionea hali halisi ya upatikanaji wa maji na kutafuta suluhisho katika maeneo yenye changamoto za kihuduma zinazowakabili wananchi.

“Huduma ya Maji katika eneo letu la kihuduma Dar na Pwani iko vizuri na leo tunapita mitaani kukagua na kujiridhisha upatikanaji wa huduma tunayozalisha kama inawafikia wananchi na iwapo kama kuna changamoto basi tunazitatua na wananchi wanaendelea kufurahia huduma” amesema Mhandisi Bwire.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Kinyerezi, Hassan Hamiss Nandeta, ameishukuru DAWASA kwa hatua madhubuti ilizochukua katika kuboresha huduma ya maji safi kwenye maeneo yao, akibainisha kuwa wananchi wameanza kunufaika na maboresho hayo.

DAWASA inaendelea kutekeleza mkakati wa kuboresha huduma za maji safi na usafi wa mazingira kwa wakazi wa Dar es Salaam na maeneo jirani, ikiwa ni sehemu ya dhamira yake ya kuhakikisha kila mteja anapata huduma bora na ya uhakika.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...