Simba, Yanga zaondoka nchini

Na Winfrida Mtoi

Timu za Simba na Yanga leo zimeondoka nchini leo kwa ajili ya kwenda kucheza michezo yao raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga imeelekea Angola, kuikabili  Wiliete ya nchini humo Septemba 19, 2025, Uwanja wa  11 de Novembro, huku Simba ikitarajiwa kutua Botswana ambapo  itacheza na Gaborone United Septemba 20, 2025 kwenye dimba la Obed Itani Chilume.

Vigogo hao wa soka nchini wenye maskani yao Kariakoo jijini Dar es Salaam, wameondoka baada ya jana kucheza mechi ya Ngao ya Jamii na Yanga kutwaa ubingwa huo.

Baada ya mechi hizo zitarejea nchini kujiandaa na michezo ya marudiano ambapo Yanga na Wiliete zitarudiana Septemba 27, 2025, Benjamin Mkapa.  Simba itarudiana na Gaborone United Septemba 28,2025 kwenye uwanja huo huo.

spot_img

Latest articles

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

More like this

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...