INEC yamteua Mpina kugombea Urais

Na Winfrida Mtoi

TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imemteua rasmi  Luhaga Mpina kuwa Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia Chama Cha ACT Wazalendo katika uchaguzi  mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Mpina ameteuliwa pamoja na mgombea mwenza wake, Fatma Abdulhabib  Ferej, ambapo leo Septemba 13, 2025 walifika katika Ofisi Ndogo za INEC  na  kukabidhiwa  fomu ya uteuzi na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele.

Katika tukio hilo, Mpina aliambatana na viongozi mbalimbali waandamizi wa chama hicho pamoja na wafuasi waliokuwa wakishangilia hatua ya chama chao kufanikisha uteuzi huo.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza mbele ya viongozi wa ACT Wazalendo.
Baadhi ya viongozi wa ACT Wazalendo wakiwa katika uteuzi wa mgombea Urais wa chama chao

Akizungumzia uteuzi huo, Mpina amesema hatua ya INEC kuwateua rasmi inaashiria kuwa safu yao imekamilika na watashirikiana kuhakikisha wanatumia siku za kampeni zilizobaki kufikia majimbo yote ya Tanzania.

Mpina amerejesha  fomu ikiwa ni siku mbili baada ya kushinda kesi ya kupinga kuenguliwa  kwenye mchakato wa uteuzi wa wagombea.

spot_img

Latest articles

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

More like this

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...