DC Msando aridhishwa uzalishaji maji Ruvu, atoa maagizo Dawasa

Na Mwandishi Wetu

MKUU cmwa Wilaya ya Ubungo (DC), Albert Msando amefanya ziara katika mtambo wa uzalishaji maji Ruvu Juu kwa lengo la kuona na kujiridhisha hali ya uzalishaji wa maji katika mtambo huo ambao unahudumia sehemu kubwa ya Wilaya ya Ubungo.

Katika ziara yake hiyo aliyoambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Ubungo pamoja na watendaji wa Dawasa, DC Msando ameridhishwa na hali ya uzalishaji maji huku akitoa maagizo kwa DAWASA kutatua changamoto zilizopo kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji.

“Tumefika hapa Ruvu Juu na tumejiridhisha uzalishaji wa maji upo vizuri, tunafahamu kulikuwa na matengenezo yanaendelea na kusababisha baadhi ya maeneo kukosa maji tumeona matengenezo yamekamilika na huduma inarejea kwa wananchi,” amesema Msando.

Msando ametoa maagizo kwa watendaji wa DAWASA hasa waliopo Wilaya ya Ubungo kuhakikisha maji yanayozalishwa yanawafikia wananchi bila kikwazo na kutoa taarifa kwa wakati pale panapotokea changamoto yeyote ya huduma lakini zaidi wanaopata maji kwa migao wajue siku gani wanapata na ratiba hiyo isimamiwe bila kupindishwa.

“Nirudie kusema tena, swala la upotevu wa maji halikubaliki, Serikali inatumia gharama kubwa kuchakata maji haya mpaka yanapomfikia mteja uwekezaji huu lazima uthaminiwe na tusimamie vyema kila mwananchi apate maji,” amesema Msando.

Meneja wa Mtambo wa uzalishaji maji Ruvu Juu, Mhandisi Juma Kasekwa amesema kwasasa hali ya uzalishaji imerejea katika hali ya kawaida na maeneo yaliyokuwa hayapati maji, huduma inaendelea kuimarika.

“Katika hali ya kuboresha uzalishaji maji katika mtambo wetu wa Ruvu Juu, Serikali imetupatia zaidi ya Shilingi bilioni 1 kununua pampu mbili mpya ambazo ni mategemeo yetu mpaka ifikapo mwezi Novemba tutakua tumezifunga na Kuongeza uzalishaji wa maji,” amesema Kasekwa.

spot_img

Latest articles

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

📌Waziri Ndejembi ashuhudia utiaji saini, asema ni alama ya miradi ya kielelezo nchini 📌Mradi utakuwa...

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius J. Ndejembi, leo Julai 27, 2026, ameshuhudia...

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

More like this

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

📌Waziri Ndejembi ashuhudia utiaji saini, asema ni alama ya miradi ya kielelezo nchini 📌Mradi utakuwa...

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius J. Ndejembi, leo Julai 27, 2026, ameshuhudia...

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...