Ratiba ya Ligi Kuu msimu wa 2025/26 hadharani, Dabi ya Kariakoo Des 13

Na Winfrida Mtoi

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara(TPLB) leo  Agosti 29, 2025,  imetangaza ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ya 2025/26, ikitarajia kuanza rasmi Septemba 17, 2025 na kutamatika Mei 23, 2026,  huku mchezo wa Dabi ya Karikoo Yanga dhidi ya Simba utapigwa Desemba  13, 2025, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Mchezo wa raundi ya pili wa watani hao wa jadi ambao mwenyeji atakuwa Simba, utapigwa Aprili 04,2026 kwenye dimba uwanja huo.

Mechi za ufunguzi za msimu huu mpya, KMC itaikaribisha Dodoma Jiji Uwanja wa KMC Complex, Mwenge wakati Coastal Union itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons katika dimba la Mkwakwani, Tanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPLB, Ibrahim Mwayela amesema ratiba hiyo imezingatia kalenda ya mashindano yote ya ndani na Kimataifa ili kuhakikisha ligi hiyo inakwenda vizuri na kumalizika Mei 23, 2026 kama ilivyopangwa.

 “Ligi yetu inakwenda kuanza rasmi. Tunaamini utakuwa ni msimu mzuri wenye ushindani mkubwa kwa sababu timu zote zimejiandaa na zimesajili vizuri sana na maandalizi yanaendelea,” amesema.

Ratiba yote ya Ligi Kuu Tanzania Bara hii hapa https://www.ligikuu.co.tz

spot_img

Latest articles

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

Waangalizi wa Uchaguzi watakiwa kutoingilia mchakato wa Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAANGALIZI wa Uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wametakiwa kuzingatia sheria...

More like this

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...