Polisi feki wakamatwa Pemba

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kujifanya askari Polisi wa kitengo cha uchunguzi wa magari yaliyoibiwa.

Watuhumiwa hao ni Abdulkadir Uwiso (55) mfanyakazi wa kampuni ya ulinzi na mkazi wa Buza na Khalfani Molo (60) mfanyabiashara wa Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi Mkoa Kaskazini Pemba, watu hao walifika katika Kijiji cha Konde na kujitambulisha kuwa ni maafisa wa Polisi kutoka Makao Makuu ndogo ya Polisi Dar es Salaam, kitengo cha uchunguzi wa magari yaliyoibiwa.

Taarifa hiyo inasema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika Stendi ya Konde wakiwa tayari wamekamata gari moja ya abiria aina ya Coaster yenye namba za usajili Z510MY ambapo walimtaka dereva wa gari hiyo, Said Nassor Ali kituoni wakidai ni gari la wizi lililoibiwa Msumbiji.

Baada ya watuhumiwa kufanyiwa upekuzi walikutwa na redio call moja, funguo ya pingu na filimbi ya Jeshi la Polisi.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...