Polisi feki wakamatwa Pemba

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kujifanya askari Polisi wa kitengo cha uchunguzi wa magari yaliyoibiwa.

Watuhumiwa hao ni Abdulkadir Uwiso (55) mfanyakazi wa kampuni ya ulinzi na mkazi wa Buza na Khalfani Molo (60) mfanyabiashara wa Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi Mkoa Kaskazini Pemba, watu hao walifika katika Kijiji cha Konde na kujitambulisha kuwa ni maafisa wa Polisi kutoka Makao Makuu ndogo ya Polisi Dar es Salaam, kitengo cha uchunguzi wa magari yaliyoibiwa.

Taarifa hiyo inasema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika Stendi ya Konde wakiwa tayari wamekamata gari moja ya abiria aina ya Coaster yenye namba za usajili Z510MY ambapo walimtaka dereva wa gari hiyo, Said Nassor Ali kituoni wakidai ni gari la wizi lililoibiwa Msumbiji.

Baada ya watuhumiwa kufanyiwa upekuzi walikutwa na redio call moja, funguo ya pingu na filimbi ya Jeshi la Polisi.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...