Yanga yafuta taarifa ya ufafanuzi wa milioni 100, Chadema yawajia juu viongozi wa klabu

Na Mwandishi Wetu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewataka viongozi wa klabu ya  Yanga, kutathmini uhalali wao wa kuongoza klabu hiyo kwa kitendo cha kukichangia Chama Cha Mapinduzi (CCM)  sh 100 milioni.

Taarifa ya Chadema iliyotolewa leo tarehe 15 Agosti 2025, na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa  Chadema, Brenda Rupia.

Katika taarifa hiyo Rupia ameeleza kuwa kitendo cha Yanga kuichangia CCM ni dharau kwa wanachama na mashabiki wenye itikadi za vyama mbalimbali za siasa.

Rupia ameeleza kuwa taarifa ya yanga ya kudai kuwa mchango huo ulitoka kwa GSM haikuwa ya kweli kwa kuwa taarifa za awali zilidai kuwa GSM, amechangia sh.10 Bilioni, huku Yanga ikichangia sh.100 milioni.

Katika hatua nyingine Yanga imeondoa katika mitandao yake ya kijamii  taarifa ya ufafanuzi waliyoandika kwa Umma jana juu ya mchango huo, pamoja na kuwaomba radhi mashabiki waliyoitoa jana Agosti 14,2025.

spot_img

Latest articles

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

More like this

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...