CCM yaomba kuchangiwa bilioni 100 za kampeni

Na Mwandishi Wetu

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinahitaji kupata sh 100 bilioni kwa ajili ya shughuli za kampeni kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akizungumza na waandishi na wahariri wa habari leo Agosti 11,2025, jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa CCM ambaye pia ni mgombea mwenza wa Urais, Dk. Emmanuel Nchimbi ameviomba vyama shindani vya siasa kuichangia CCM sambamba na wanachama na wadau wengine.

Amesema harambee ya kuchangia kampeni za chama hicho inatarajia kuzinduliwa rasmi kesho katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ikiwa ni kwa ajili ya maandalizi ya kampeni katika kugharamia magari, mabango, mafuta, fulana na kanga.

Dk. Nchimbi amesema uamuzi wa kuandaa harambee hiyo umetokana na hamasa kubwa iliyojitokeza kwa wanachama kutaka kuchangia kampeni.

“Kwa wakati ule kulitokea hamasa kubwa kwa wanachama wa CCM kutamani kuchangia michango ya kampeni. Kutokana na hamasa hiyo, sisi kama Kamati Kuu tumeamua sasa kuwashirikisha wanachama wetu katika uchangiaji kesho saa 11 jioni katika ukumbi wa Mlimani City,”


Vilevile, Dk. Nchimbi amefungua milango kwa vyama vingine kuchangia katika kampeni hiyo ambapo amesema kuwa;

“Kuhusu vyama vingine, tutafarijika sana vikichangia, kwa sababu haihitaji ushahidi wa kipolisi kujua CCM inatumikia watanzania na vyama vingine vyote,”

Akizungumzia kuhusu udhibiti wa fedha haramu, amesema “Jitihada yetu kubwa sisi kama CCM ni kujiepusha kuwa Serikali, kwa hiyo sisi siyo taasisi ya uchunguzi wa fedha haramu. Wenye kazi yao wataendelea kutafuta fedha hizo, sisi tutaendelea kufanya kazi ya siasa, kwa maana kitu kinachoharibu nchi ni chama cha siasa kuendelea kufanya kazi za dola,” ameeleza.

spot_img

Latest articles

Jeshi la Polisi latoa onyo wanaondelea kuhamasisha maandamano

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi nchini limesema  kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi...

Watanzania waaswa kudumisha amani, Umoja na mshikamano

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika, Watanzania wametakiwa kukumbuka...

Serikali kuanzisha Kituo Maalum cha Wawekezaji Vijana

Na Tatu Mohamed SERIKALI inatarajia kuanzisha kituo Maalum cha kuhudumia na kuwezesha wawekezaji vijana(Youth Investors...

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

More like this

Jeshi la Polisi latoa onyo wanaondelea kuhamasisha maandamano

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi nchini limesema  kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi...

Watanzania waaswa kudumisha amani, Umoja na mshikamano

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika, Watanzania wametakiwa kukumbuka...

Serikali kuanzisha Kituo Maalum cha Wawekezaji Vijana

Na Tatu Mohamed SERIKALI inatarajia kuanzisha kituo Maalum cha kuhudumia na kuwezesha wawekezaji vijana(Youth Investors...