Rais wa Yanga akatwa uteuzi Jimbo la Kigamboni, Jemedali, Shafii Dauda mambo mazuri

Na Mwandishi Wetu

Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Hersi Saidi ameshindwa kupenya katika  uteuzi wa awali wa wagombea ubunge  Jimbo la Kigamboni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku wadau wengine wa michezo wakiwamo wachambuzi wa soka, Shafii Dauda na Jemedali Said wakipita.

Injinia Hersi jina lake halikuwepo kati ya wagombea sita walioteuliwa kwa jimbo la Kigamboni ambao ni Ponela Matei, Habib Mchange, Allan Sanga, Henjelewe, Ally Mandai na Francis Elias.

Kwa upande wa Jemedali ametishwa na Chama hicho katika Jimbo la Mtama, mkoani Lindi akiwa pamoja na Nape Nnauye, Jabir Chilumba na Meta Nahonyo wakati Shafii Dauda akiteuliwa Jimbo la Temeke, jijini Dar es Salaam akiwa na Mariam Nassoro, Dorothy Kilave, Bernard Mwakyembe, Fadhil, Leah Mwampishi na Mussa Ntulia.

 Wanamichezo wengine walipita  katika uteuzi huo wa awali, ni Msemaji wa Azam Fc, Hasheem Ibwe, Jimbo la Mwanga, wakati Revocatus  Chiponda ‘Baba Levo’ akipenya Jimbo la Kigoma.

Majina ya wateule katika majimbo mbalimbali  wa CCM, yamewasilishwa  kwa waandishi wa habari leo Julai  29,2025 jijini Dodoma na  Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa  chama hicho, Amos Makalla.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...