Rais wa Yanga akatwa uteuzi Jimbo la Kigamboni, Jemedali, Shafii Dauda mambo mazuri

Na Mwandishi Wetu

Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Hersi Saidi ameshindwa kupenya katika  uteuzi wa awali wa wagombea ubunge  Jimbo la Kigamboni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku wadau wengine wa michezo wakiwamo wachambuzi wa soka, Shafii Dauda na Jemedali Said wakipita.

Injinia Hersi jina lake halikuwepo kati ya wagombea sita walioteuliwa kwa jimbo la Kigamboni ambao ni Ponela Matei, Habib Mchange, Allan Sanga, Henjelewe, Ally Mandai na Francis Elias.

Kwa upande wa Jemedali ametishwa na Chama hicho katika Jimbo la Mtama, mkoani Lindi akiwa pamoja na Nape Nnauye, Jabir Chilumba na Meta Nahonyo wakati Shafii Dauda akiteuliwa Jimbo la Temeke, jijini Dar es Salaam akiwa na Mariam Nassoro, Dorothy Kilave, Bernard Mwakyembe, Fadhil, Leah Mwampishi na Mussa Ntulia.

 Wanamichezo wengine walipita  katika uteuzi huo wa awali, ni Msemaji wa Azam Fc, Hasheem Ibwe, Jimbo la Mwanga, wakati Revocatus  Chiponda ‘Baba Levo’ akipenya Jimbo la Kigoma.

Majina ya wateule katika majimbo mbalimbali  wa CCM, yamewasilishwa  kwa waandishi wa habari leo Julai  29,2025 jijini Dodoma na  Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa  chama hicho, Amos Makalla.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...