Gambo aenguliwa, CCM yateua watia nia saba kura za maoni Arusha Mjini

Na Mwandishi Wetu

KAMATI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imewateua watia nia saba kuingia katika mchakato wa kura za maoni kwa nafasi ya Ubunge wa Arusha Mjini, huku Mbunge wa sasa, Mrisho Gambo, akiwekwa kando.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 29, 2025 Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ametaja majina ya watakaopigiwa kura Agosti 4, 2025, ni Ally Babu, Hussein Gonga, Aminata Taure, Mustafa Nasoro, Paul Makonda, Rwembo Mgweno na Jasper Kishumbua.

Gambo, ambaye aliingia bungeni kwa kipindi cha kwanza kupitia jimbo hilo, hatakuwa sehemu ya mchakato huo.

Kabla ya ubunge, alihudumu kama Mkuu wa Mkoa wa Arusha, nafasi ambayo ilimuweka karibu na siasa za mkoa huo kwa muda mrefu.

spot_img

Latest articles

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

More like this

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...