Gambo aenguliwa, CCM yateua watia nia saba kura za maoni Arusha Mjini

Na Mwandishi Wetu

KAMATI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imewateua watia nia saba kuingia katika mchakato wa kura za maoni kwa nafasi ya Ubunge wa Arusha Mjini, huku Mbunge wa sasa, Mrisho Gambo, akiwekwa kando.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 29, 2025 Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ametaja majina ya watakaopigiwa kura Agosti 4, 2025, ni Ally Babu, Hussein Gonga, Aminata Taure, Mustafa Nasoro, Paul Makonda, Rwembo Mgweno na Jasper Kishumbua.

Gambo, ambaye aliingia bungeni kwa kipindi cha kwanza kupitia jimbo hilo, hatakuwa sehemu ya mchakato huo.

Kabla ya ubunge, alihudumu kama Mkuu wa Mkoa wa Arusha, nafasi ambayo ilimuweka karibu na siasa za mkoa huo kwa muda mrefu.

spot_img

Latest articles

Okello awapa jeuri mashabiki wa Yanga

Na Mwandishi Wetu Nyota wa Yanga, Allan Okello amewahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa watamaliza...

Minziro akabidhiwa Fountain Gate FC

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Fountain Gate FC imemtangaza Fred Felix Minziro kuwa Kocha Mkuu...

Makonda asimamisha uongozi TOC, Rage akabidhiwa jukumu

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesimamisha uchaguzi wa...

Nani amwambie Rais Samia: ‘Name and Shame’ bila vyombo vya habari imara haifui dafu

SUALA la utawala bora halijawahi kuwa eneo rahisi katika uendeshaji na usimamizi wa ofisi...

More like this

Okello awapa jeuri mashabiki wa Yanga

Na Mwandishi Wetu Nyota wa Yanga, Allan Okello amewahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa watamaliza...

Minziro akabidhiwa Fountain Gate FC

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Fountain Gate FC imemtangaza Fred Felix Minziro kuwa Kocha Mkuu...

Makonda asimamisha uongozi TOC, Rage akabidhiwa jukumu

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesimamisha uchaguzi wa...