Gambo aenguliwa, CCM yateua watia nia saba kura za maoni Arusha Mjini

Na Mwandishi Wetu

KAMATI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imewateua watia nia saba kuingia katika mchakato wa kura za maoni kwa nafasi ya Ubunge wa Arusha Mjini, huku Mbunge wa sasa, Mrisho Gambo, akiwekwa kando.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 29, 2025 Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ametaja majina ya watakaopigiwa kura Agosti 4, 2025, ni Ally Babu, Hussein Gonga, Aminata Taure, Mustafa Nasoro, Paul Makonda, Rwembo Mgweno na Jasper Kishumbua.

Gambo, ambaye aliingia bungeni kwa kipindi cha kwanza kupitia jimbo hilo, hatakuwa sehemu ya mchakato huo.

Kabla ya ubunge, alihudumu kama Mkuu wa Mkoa wa Arusha, nafasi ambayo ilimuweka karibu na siasa za mkoa huo kwa muda mrefu.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...