Gavana Tutuba azindua Jarida la Uchumi Wetu, Toleo Namba 1

Na Mwandishi Wetu

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutuba, amezindua rasmi Jarida la Uchumi Wetu, Toleo Namba 1 la Julai, 2025 linaloandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania kupitia Idara ya Mawasiliano kila baada ya miezi mitatu.

Akizungumza katika uzinduzi wa Jarida hilo Gavana Tutuba alipongeza kazi nzuri inayofanywa na Idara hiyo katika kuhabarisha umma kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu uchumi wa Tanzania.

Ameongeza kuwa Jarida hilo litakuwa ni wenzo wa kuuwezesha umma kusoma habari zihusuzo sekta ya fedha na uchumi wa nchi kiujumla zinazotoka Benki Kuu, Serikalini pamoja na sekta binafsi.

Jarida la Uchumi Wetu limesheheni maarifa kupitia habari, makala na matukio mbalimbali na litasambazwa kwa njia ya nakala tepe (soft copies) kupitia tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania www.bot.go.tz.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...