Fountain Gate FC yakwepa kushuka daraja

Na Mwandishi Wetu

Klabu ya Fountain Gate  imefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu  Tanzania Bara kwa msimu ujao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Stand United katika mchezo wa mtoano uliopigwa kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, mkoani Manyara.

Fountain Gate meshinda jumla ya mabao 5-1 katika michezo miwili ya mtoano  ya nyumbani na ugenini baada ya kushinda 3-1 katika mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga na leo wakahitimisha kwa ushindi wa 2-0 nyumbani.

Mabao ya leo yamefungwa na Elie Mkono dakika ya 51 na Edger William dakika ya 90, hivyo kuihakikishia timu hiyo nafasi ya kuendelea kusalia  kwa msimu wa 2025/2026.

Ushindi huo umeleta furaha kwa mashabiki wa  timu hiyo kutokana na  kukwepa kushuka daraja kupitia  hatua ya mtoano.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

More like this

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...