Fountain Gate FC yakwepa kushuka daraja

Na Mwandishi Wetu

Klabu ya Fountain Gate  imefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu  Tanzania Bara kwa msimu ujao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Stand United katika mchezo wa mtoano uliopigwa kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, mkoani Manyara.

Fountain Gate meshinda jumla ya mabao 5-1 katika michezo miwili ya mtoano  ya nyumbani na ugenini baada ya kushinda 3-1 katika mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga na leo wakahitimisha kwa ushindi wa 2-0 nyumbani.

Mabao ya leo yamefungwa na Elie Mkono dakika ya 51 na Edger William dakika ya 90, hivyo kuihakikishia timu hiyo nafasi ya kuendelea kusalia  kwa msimu wa 2025/2026.

Ushindi huo umeleta furaha kwa mashabiki wa  timu hiyo kutokana na  kukwepa kushuka daraja kupitia  hatua ya mtoano.

spot_img

Latest articles

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

More like this

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...