TMDA yaendelea kuelimisha umma juu ya matumizi sahihi ya dawa Sabasaba

Na Tatu Mohamed

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Imeendelea kutoa Elimu kwa Umma juu ya matumizi sahihi ya Dawa na vitenganishi ndani ya maonesho ya 49 ya Kimataifa ya biashara (SabaSaba) yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Temeke, Dar Es Salaam.

Akizungumza katika banda la Stone town ndani ya maonesho hayo ya Sabasaba, Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo amesema kama Mamlaka mara kwa mara wataendelea kutoa elimu kwa Umma ili kusaidia Jamii kuwa na uelewa wa matumizi sahihi ya Dawa.

Amesema majukumu makubwa ya TMDA ni kusajili dawa za ndani na zinazotoka nje kuingia nchini hii ni pamoja na kufanya ukaguzi kila siku ikiwemo kwenye maduka ya Dawa, masoko na mipaka ili kumlinda mtanzania.

“Sisi jukumu letu kuhakikisha kwamba dawa inatumika kama ilivyokusudiwa na sio kumdhuru mtumiaji.Majukumu yetu ni kuhakikisha tunasajili dawa zilizosajiliwa na kukidhi soko la nchi yote hii ni kumlinda Mtanzania katika usalama wa dawa hivyo tunahakika ubora na ufanisi.

“Vile vile tunafanya kazi tunapima bidhaa za dawa kupitia Maabara zetu za kisasa ambazo zina ubora wa Kimataifa wa WHO,” amesema Dkt. Adam Fimbo.

Aidha, katika banda hilo la TMDA, Dkt Adam Fimbo ametoa elimu kwa Wananchi waliotembelea juu ya matumizi sahihi ya Dawa na kuacha kutumia bidhaa hiyo kiholela bila kufuata maelekezo na ushauri wa wataalamu ili kuepuka usugu wa dawa.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...