Na Winfrida Mtoi
Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Debora Mwenda, ametangaza vita dhidi ya mpinzani wake Asia Meshack , akiahidi kulipa kisasi katika pambano la Dar Boxing Derby litakalofanyika Julai 26, 2025, jijini Dar es Salaam.
Amesema pambano lililopita baada ya kupoteza alipata hasira kali hadi kulia ulingoni, hivyo bado ana machungu na hasira zote atazimaliza mchezo ujao watakapokutana tena na mpinzani wake.
“Nimuambie tu mpinzani wangu Asia kuwa bado nina hasira ya mechi niliopoteza mbele yake na nililia. Namuambia ajipange maana hiyo hasira iliyonifanya ya nilie itakuja kumuishia yeye,” ametamba Debora.

Amesema mashabiki wake watarajie kuona mabadiliko ulingoni kwa kuwa amejipanga kuwapa burudani na kuondoka na ushini siku hiyo.
Hata hivyo amekiri kuwa mpinzani wake ni mzuri lakini amejiandaa vizuri kuhakikisha hawezi kurudia makosa yaliyomfanya apoteze pambano lililopita.