Bondia Debora amtangazia vita Asia, apania kulipa kisasi

Na Winfrida Mtoi

Bondia  wa ngumi za kulipwa nchini, Debora Mwenda, ametangaza vita dhidi ya mpinzani wake Asia Meshack , akiahidi kulipa kisasi katika pambano la Dar Boxing Derby litakalofanyika Julai 26, 2025, jijini Dar es Salaam.

Amesema  pambano lililopita baada ya kupoteza alipata hasira kali hadi kulia ulingoni, hivyo bado ana machungu na hasira zote atazimaliza  mchezo ujao watakapokutana  tena na mpinzani wake.

“Nimuambie tu mpinzani wangu Asia kuwa bado nina hasira  ya mechi niliopoteza mbele yake na  nililia.  Namuambia ajipange maana hiyo hasira iliyonifanya ya nilie itakuja kumuishia yeye,” ametamba Debora.

Amesema mashabiki wake watarajie kuona mabadiliko ulingoni kwa kuwa amejipanga kuwapa burudani na kuondoka na ushini siku hiyo.

Hata hivyo amekiri kuwa mpinzani wake ni mzuri lakini amejiandaa vizuri kuhakikisha hawezi kurudia makosa yaliyomfanya apoteze pambano lililopita.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...