Wasira: Uchaguzi Mkuu sio ajali

Na Mwandishi Wetu

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amewaeleza wabunge na madiwani hususan waliokuwa wanajifungia vioo kwenye magari wajue wakati umefika.

Amesema uchaguzi mkuu sio ajali na kwamba wabunge na madiwani wanajua kila baada ya miaka mitano hufanyika uchaguzi mkuu.

Aidha, amewaeleza wana CCM wanaotaka kugombea ubunge na udiwani ni vema wakapima uwezo wao kama ambavyo unapaswa kupima kina cha maji kwa fimbo kabla ya kuvuka mto kusombwa na maji.

Akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM katika Wilaya ya Magu mkoani Mwanza, leo Juni 23, 2025, Wasira ametumia nafasi hiyo kuwataka wana CCM kujiandaa kwenda kutiki ifikapo Oktoba na kwa nafasi ya urais tayari Chama kimepitisha jina la Dk. Samia Suluhu Hassan na mgombea mwenza ni Dk. Emanuel Nchimbi.

“Kwa upande wa urais tumemaliza tumeshaweka mgombea wetu Dk.Samia Suluhu Hassan na kazi yetu ni kumuuza kwa wananchama na wananchi .Kwa wabunge kama ubunge unaisha Juni 27 ndio maana hauwapi presha maana tangu walipoingia maana walijua ikifika miaka mitano uchaguzi unafanyika.

“Kwa hiyo uchaguzi sio ajali kama wewe unauogopa labda hukufanya maandalizi maana wako watu katika jamii hata wale waliowachagua hawawajui wale ndio wenye kupata presha… sasa kama unafunga vioo unawapita watu usilaumu watu,” amesema.

Ameeleza kuwa amekuwa bungeni kwa miaka 30, hivyo analijua bunge vizuri na kueleza kwamba ubunge unavyopatikana unapatikana kwa kujenga uhusiano na watu, ukijenga uhusiano na watu mambo yako yanakuwa rahisi

“Kazi yangu si kumpigia mtu debe mbunge ila ukifika kwa wana wana CCM na lakini ukifika hapa kwa mfano unasikia kaulimbiu za wananchi au wana CCM wanamtaja wanayemtaka.Kwa wabunge ambao walifanya kazi zao vizuri wala hawana wasiwasi,” ameeleza Wasira.

 Pia Wasira amesema uchaguzi umefika na wanachama wana haki ya kuchukua fomu ila alishauri kwa wale wanachama wapya wanaotaka ubunge wakapima nguvu ya waliopo au waliomaliza muda wao.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...