Dk. Mpango ashiriki Misa Takatifu iliyoongozwa na Papa Leo XIV, atembelea kampuni ya Health 3000

Na Mwandishi Wetu

Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango na mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameungana na waumini mbalimbali wa Kanisa Katoliki Duniani kushiriki Dominika ya Ekaristi Takatifu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohana wa Laterano lililopo Roma nchini Italia.

Misa hiyo imeongozwa na Papa Leo XIV. Makamu wa Rais yupo nchini Italia kumwakilisha Rais  Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na mikutano mbalimbali ya uwili.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais  ametembelea Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji wa Vifaa Tiba ya Health 3000 jijini Roma, Italia.

Katika ziara hiyo, Dk. Mpango amefanya mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo, wakiongozwa na Mwenyekiti Maurizio Flammini na Mkurugenzi Mtendaji, Eleonora Flammini. Mazungumzo yao yakilenga kuimarisha ushirikiano katika sekta ya afya, hususani kwenye matibabu kwa njia ya mtandao (telemedicine).

Health 3000 ni mojawapo ya kampuni zilizo chini ya FG Group, inayojikita katika uzalishaji wa vifaa tiba kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Dk. Mpango yupo nchini Italia kumwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan), pamoja na mikutano mingine ya ‘uwili’.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...