Dk. Mpango ashiriki Misa Takatifu iliyoongozwa na Papa Leo XIV, atembelea kampuni ya Health 3000

Na Mwandishi Wetu

Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango na mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameungana na waumini mbalimbali wa Kanisa Katoliki Duniani kushiriki Dominika ya Ekaristi Takatifu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohana wa Laterano lililopo Roma nchini Italia.

Misa hiyo imeongozwa na Papa Leo XIV. Makamu wa Rais yupo nchini Italia kumwakilisha Rais  Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na mikutano mbalimbali ya uwili.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais  ametembelea Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji wa Vifaa Tiba ya Health 3000 jijini Roma, Italia.

Katika ziara hiyo, Dk. Mpango amefanya mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo, wakiongozwa na Mwenyekiti Maurizio Flammini na Mkurugenzi Mtendaji, Eleonora Flammini. Mazungumzo yao yakilenga kuimarisha ushirikiano katika sekta ya afya, hususani kwenye matibabu kwa njia ya mtandao (telemedicine).

Health 3000 ni mojawapo ya kampuni zilizo chini ya FG Group, inayojikita katika uzalishaji wa vifaa tiba kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Dk. Mpango yupo nchini Italia kumwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan), pamoja na mikutano mingine ya ‘uwili’.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...