Kinyozi ahukumiwa  kifungo cha miaka 30 jela kwa kubaka mwanafunzi

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Kwimba imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela kinyozi wa saluni ya kiume, Lindwa Clement Balthazari (30), mkazi wa kijiji cha Malya  baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 14 kutoka Shule ya Msingi Mwakulilima.

Hukumu hiyo imesomwa leo, Juni 17, 2025, na Hakimu Mkazi Mfawidhi Ndeko Dastan katika kesi ya jinai namba 31961/2024, baada ya mahakama kuridhika na ushahidi wa upande wa Jamhuri.

Mshtakiwa alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Desemba 4, 2024, na kusomewa shtaka la kubaka na Wakili wa Serikali Juma Kiparo, ambapo alikana kutenda kosa hilo.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, Lindwa alitenda kosa hilo nyumbani kwake kwa nyakati tofauti mwezi Oktoba 2024, akitumia nafasi ya kumhudumia mtoto huyo kwenye saluni yake kabla ya kumrubuni na kumbaka, kinyume na vifungu vya sheria 130(1), 130(2)(e), na 131(1) vya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 (marejeo ya 2022).

Upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi wanne, wakiwemo mhanga na daktari, kuthibitisha pasipo shaka tuhuma hizo. Mtuhumiwa alijitetea kuwa alimchukua binti huyo kwa lengo la kumsaidia baada ya kufukuzwa nyumbani, hoja ambayo ilitupiliwa mbali na Mahakama.

Jitihada zake za kuleta mashahidi watatu kwa ajili ya utetezi hazikufua dafu, na Mahakama ikamhukumu kifungo hicho ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...

Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja...

More like this

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...