Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu

Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini India kwenda London nchini Uingereza imeanguka na kuwaka moto leo Juni 12, 2025 katika eneo la Ahmedabad India muda mfupi baada ya kupaa ikiwa na watu 242.

Kwa mujibu wa taarifa za mamlaka nchini India zimesema ndege hiyo ilikuwa imebeba  abiria 169 ni raia wa India,  raia wa  53 Uingereza, Wareno saba na raia wa Canada mmoja, huku wafanyakazi wa ndege hiyo  ni 12.

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi  kupitia mtandao wake wa kijamii wa X, amesema ameshtushwa sana na ajali hiyo ya ndege.

“Ajali ya Ahmedabad imetushtua na kutuhuzunisha. Haielezeki jinsi inavyovunja moyo, amesema Modi katika ujumbe huo alioandika.

Mtandao wa kufuatilia safari za ndege wa Flightradar24 umesema ndege hiyo ilikuwa aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, mojawapo ya ndege za kisasa zaidi zinazotumika.

spot_img

Latest articles

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...

Kweli IJP Wambura Polisi wamefanikiwa, sasa umma unataka kujua wasiojulikana

JUMATATU wiki hii Jeshi la Polisi lilikuwa na mahafali ya maofisa wa vyeo vya...

More like this

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...